Hamia kwenye habari

Watu wakichoma tairi za gari ili kufunga mtaa katika jiji la Port-au-Prince, nchini Haiti

MACHI 19, 2024
HAITI

Akina Ndugu Nchini Haiti Wanaendelea Kukabiliana na Vita vya Wenyewe kwa Wenyewe

Akina Ndugu Nchini Haiti Wanaendelea Kukabiliana na Vita vya Wenyewe kwa Wenyewe

Katika miaka ya hivi karibuni, ndugu na dada zetu nchini Haiti wameathiriwa na kuongezeka kwa jeuri inayosababishwa na magenge na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Changamoto za kisiasa na jeuri zimeongezeka sana katika mji mkuu wa Port-au-Prince, nchini Haiti, tangu Machi, 2, 2024, wakati ambapo vikundi vya watu wenye silaha walivamia na kuteka majengo fulani muhimu na maeneo mengine yanayoshughulikia huduma muhimu. Serikali imeweka vizuizi na imetangaza hali ya dharura. Ripoti zinaonyesha kwamba watu 15,000 hivi wamelazimika kukimbilia maeneo salama ya nchi na watu wengi wameuawa.

Athari Ambazo Ndugu na Dada Zetu Wamepata

  • Hakuna ndugu au dada ambaye amejeruhiwa au kuuawa

  • Ndugu na dada 113 wamelazimika kuhama makao yao

  • Nyumba 2 zimeharibiwa

  • Familia 5 zimepoteza mali zao kwa sababu ya wizi

  • Hakuna Jumba la Ufalme ambalo limeharibiwa

Jitihada za Kutoa Msaada

  • Halmashauri 4 za kutoa msaada zimeanzishwa ili kuratibu jitihada za kutoa msaada katika eneo lote la ofisi ya tawi

  • Waangalizi wa mzunguko pamoja na wazee wa makutaniko wanaandaa msaada wa kiroho na wa kimwili kwa wale ambao wameathiriwa, kutia ndani wale ambao wamelazimika kuhama kwa sababu ya vita

Tukiwa undugu wa ulimwenguni pote, tunaendelea kusali kwamba Yehova awape hekima na utulivu ndugu na dada zetu nchini Haiti katika kipindi hiki kigumu wanachokabili. Pamoja na ndugu na dada zetu wa Haiti, tunaendelea kutazamia kwa hamu utimizo wa ahadi ya Yehova ya ulimwengu mpya ambamo “amani itakuwa nyingi.”​—Zaburi 72:7.