Hamia kwenye habari

Maji ya mvua yamejaa barabarani katika mji wa Léogâne, Haiti. Picha ndogo juu: Mzee wa kutaniko akiondoa matope karibu na nyumba ya dada. Picha ndogo chini: Akina ndugu wakisafisha nyumba ya dada

JUNI 15, 2023
HAITI

Mafuriko Makubwa Yatokea Haiti

Mafuriko Makubwa Yatokea Haiti

Juni 2 na 3, 2023, mvua kubwa zilisababisha mafuriko katika sehemu mbalimbali nchini Haiti. Kulingana na ripoti zilizotolewa, maelfu ya nyumba zilijaa maji ya mvua na hivyo karibu familia 40,000 zimeathiriwa. Zaidi ya watu 13,500 wamelazimika kuhama makao yao. Watu 50 hivi wamekufa.

Athari Ambazo Ndugu na Dada Zetu Wamepata

  • Hakuna ndugu au dada aliyekufa

  • Ndugu 1 na dada 1 wamejeruhiwa

  • Wahubiri 60 wamelazimika kuhama makao yao

  • Nyumba 1 imeharibiwa kabisa

  • Nyumba 3 zimepata uharibifu mkubwa

  • Nyumba 19 zimepata uharibifu mdogo

  • Hakuna Majumba ya Ufalme au majengo yoyote ya kitheokrasi yaliyoharibiwa

Jitihada za Kutoa Msaada

  • Waangalizi wa mzunguko wanashirikiana na wazee wa makutaniko ya maeneo hayo ili kuwapa ndugu na dada zetu walioathiriwa msaada wa kiroho na wa kimwili

  • Makutaniko yaliyo katika maeneo hayo yanasaidia katika jitihada za kutoa msaada

Tuna uhakika kwamba “Yehova atawapa nguvu” ndugu na dada zetu walioathiriwa na mafuriko hayo yaliyotokea Haiti.​—Zaburi 29:11.