Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Endeleeni Kukesha!”

“Endeleeni Kukesha!”

“Endeleeni Kukesha!”

Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova

▪ Maelfu ya makusanyiko haya ya siku tatu ambayo yamepangiwa kuanza Marekani kwenye mwisho juma wa Mei 22-24 (Mwezi wa 5), yatafanywa ulimwenguni pote kwa miezi kadhaa itakayofuata. Huko Marekani, kila siku vipindi vitaanza kwa programu ya muziki saa 3:20 asubuhi. Kichwa kikuu cha Ijumaa (Siku ya 5) kinachotegemea andiko la Mathayo 24:44 ni “Iweni Tayari.” Hotuba ya mwenyekiti itafuatwa na hotuba “Makusanyiko Hutusaidia Kukesha” na hotuba “Yehova—Mungu wa ‘Nyakati na Majira.’” Kisha mfululizo wenye kichwa “Waige Waaminifu Walioendelea Kukesha” utazungumzia jinsi Noa, Musa, na Yeremia walivyofanya hivyo. Programu ya asubuhi itamalizika kwa hotuba ya msingi yenye kichwa “Jinsi Yehova Anavyotusaidia ‘Kuendelea Kukesha.’”

Sehemu ya kwanza Ijumaa alasiri ina kichwa “Majibu ya Maswali Kuhusu ‘Siku za Mwisho,’” itakayofuatwa na hotuba “‘Hamwijui Ile Siku Wala Saa’—Kwa Nini?” na hotuba “Jueni Kwamba Mwisho Uko Karibu.” Kisha kutakuwa na mfululizo wenye sehemu sita wenye kichwa “Enyi Familia za Kikristo, ‘Kaeni Macho’!” Sehemu tatu za kwanza zinaelekezwa moja kwa moja kwa waume, wake, na vijana. Nazo sehemu tatu za mwisho zina vichwa “Uwe na Jicho Rahisi,” “Endeleeni Kufuatilia Malengo ya Kiroho,” na “Endeleeni Kufanya Ibada ya Familia.” Kipindi cha alasiri kitamalizika kwa hotuba “Mistari Inayotuchochea Kuwa Waangalifu.”

Kichwa kikuu Jumamosi (Siku ya Posho) ni “Tunzeni Akili Zenu, Iweni Wenye Kulinda,” kinachotegemea 1 Petro 5:8. Mfululizo wenye sehemu tano “Wasaidie Watu ‘Waamke Kutoka Katika Usingizi,’” utakuwa na hotuba “Huduma Yetu—Kwa Nini Ni Muhimu Sana?,” “Uwe Mtambuzi Katika Huduma,” “Jitahidi Kuboresha Ustadi Wako,” “Usiwasahau Watu wa Ukoo!,” na “Dumisha Bidii Yako!” Baada ya hotuba “Iga Mfano wa Yesu wa Kukesha” na hotuba “Endelea Kukesha Kuhusiana na Sala,” kipindi hicho kitamalizika kwa hotuba ya ubatizo, na baada ya hapo wale wanaostahili watabatizwa.

Programu ya Jumamosi alasiri itakuwa na mfululizo wenye sehemu tano wenye kichwa “Uwe Macho Kuhusu Mitego ya Shetani!”—“Moto,” “Shimo,” “Mtego,” “Mtego Unaofisha,” na “Mtego Unaoponda.” Mfululizo huo utafuatwa na sehemu ya pekee yenye kichwa, “Mpaka Nitakapokata Pumzi Sitajiondolea Utimilifu Wangu!” Siku hiyo itamalizika kwa hotuba “Usitazame ‘Mambo Yaliyo Nyuma.’” na “Jifunze Kukesha Kama Walivyofanya Mitume wa Yesu.”

Kichwa kikuu cha Jumapili (Siku ya Yenga) kinategemea Habakuki 2:3, “Endelea Kuyatarajia . . . Hayatachelewa.” Baada ya hotuba kuhusu kichwa kikuu cha siku hiyo, mfululizo wenye kichwa “Endeleeni Kukaza Macho Juu ya Vitu Visivyoonekana” utazungumzia mambo yafuatayo: “Zile Pembe Kumi Zitamchukia Kahaba,” “Mataifa Yatalazimika Kumjua Yehova,” “‘Falme Hizi Zote’ Zitapondwa,” “Ibilisi Atafungwa kwa Miaka Elfu,” “Watajenga Nyumba na Kupanda Mashamba ya Mizabibu,” “Mbwa-mwitu na Mwana-kondoo Watalisha Kama Kitu Kimoja,” “Mungu . . . Atafuta Kila Chozi,” “Wote Waliomo Ndani ya Makaburi ya Ukumbusho . . . Watatoka,” na “Mungu Atakuwa ‘Vitu Vyote kwa Kila Mtu.’” Kipindi cha asubuhi kitamalizika kwa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Unaweza Kuokoka Mwisho wa Dunia Jinsi Gani?”

Jumapili alasiri kutakuwa na jambo la pekee, yaani, drama ya kisasa yenye kugusa moyo yenye kichwa “Ndugu Yako Alikuwa Amekufa Naye Yuko Hai Sasa,” inayotegemea mfano wa Yesu kuhusu mwana mpotevu. Baada ya muhtasari wa funzo la kila juma la Mnara wa Mlinzi, kusanyiko litamalizika kwa hotuba “Endelea Kuitarajia na Kuingojea Siku ya Yehova!”

Fanya mipango sasa ili uhudhurie. Ili upate habari kuhusu kusanyiko ambalo litafanywa karibu nawe, tembelea Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova lililo karibu nawe au uwaandikie wachapishaji wa gazeti hili. Katika maeneo fulani kutakuwa na makusanyiko ya kimataifa ya siku nne. Gazeti la Machi 1 la Mnara wa Mlinzi, linalotolewa pamoja na gazeti hili, lina orodha ya mahali ambapo makusanyiko yatafanyiwa kutia ndani yale ya kimataifa.