Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unahesabu Gharama?

Je, Unahesabu Gharama?

Je, Unahesabu Gharama?

YESU KRISTO aliwatolea wanafunzi wake tumaini la uhai udumuo milele, na pia akawahimiza wahesabu gharama ya kuwa Wakristo. Alieleza jambo hilo kwa kuuliza: “Ni nani kati yenu atakaye kujenga mnara asiyeketi kwanza na kupiga hesabu ya gharama, ili aone kama ana kiasi cha kutosha kuukamilisha?” (Luka 14:28) Yesu alimaanisha gharama gani?

Wakristo wote hukabili majaribu—na baadhi ya majaribu hayo huwa makubwa. (Zaburi 34:19; Mathayo 10:36) Kwa hiyo, tunahitaji kujitayarisha kiakili na kiroho ili tusishangae upinzani au matatizo mengine yanapotupata. Tunapaswa kuwa tulihesabu gharama ya kuwa wanafunzi wa Kristo, tukijua kwamba thawabu tutakayopata—kukombolewa kutoka kwa dhambi na kifo—ni yenye thamani kuliko kitu chochote kinachotokana na mfumo wa sasa. Naam, hakuna kitu chochote ambacho Mungu anaruhusu—hata kifo—kinachoweza kutudhuru daima ikiwa tutaendelea kumtumikia.—2 Wakorintho 4:16-18; Wafilipi 3:8.

Imani yetu inawezaje kuwa yenye nguvu? Imani yetu hutiwa nguvu kila mara tunapofanya uamuzi unaofaa, tunapochukua msimamo thabiti kuhusiana na viwango vya Kikristo, au tunapofanya jambo linalopatana na mapenzi ya Mungu—hasa tunapokuwa chini ya mkazo wa kutenda kinyume cha mapenzi yake. Tunapopata baraka za Yehova kwa sababu ya mwenendo wetu mwaminifu, imani yetu hutiwa nguvu na kuongezeka. Kwa kufanya hivyo, tunaiga kielelezo cha Yesu, wanafunzi wake wa kwanza, na wanaume na wanawake wote waliodhihirisha imani wakati uliopita, na ambao ‘walihesabu gharama’ ya kumtumikia Mungu.—Marko 1:16-20; Waebrania 11:4, 7, 17, 24, 25, 32-38.