Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Surasak Suwanmake/Moment via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Joto Kali Kupita Kiasi la 2023—Biblia Inasema Nini?

Joto Kali Kupita Kiasi la 2023—Biblia Inasema Nini?

 Ulimwenguni pote watu wanalazimika kuvumilia joto kali sana kuliko wakati mwingine wowote bila kusahau majanga yanayosababishwa na hali mbaya ya hewa. Ona ripoti zifuatazo:

  •   “Kiwango cha joto ulimwenguni kilianza kurekodiwa miaka 174 iliyopita lakini katika kipindi hicho chote, Juni ya mwaka huu imekuwa yenye joto zaidi kuliko nyingine yoyote.”​—Shirika la Kitaifa la Usimamizi wa Bahari na Anga, Idara ya Biashara ya Marekani, Julai 13, 2023.

  •   “Italia, Hispania, Ufaransa, Ujerumani na Poland zinakabili joto kali kupita kiasi na kiwango cha joto kinatarajiwa kufika nyuzi 48 Selsiasi kwenye kisiwa cha Sicily na cha Sardinia – inaelekea hicho ndicho kiwango kikubwa zaidi cha joto kuwahi kurekodiwa barani Ulaya.”​—Shirika la Anga la Ulaya, Julai 13, 2023.

  •   “Kiwango cha joto katika sayari yetu kinapozidi kuongezeka, tunatarajia kwamba mvua zitakuwa kubwa kupita kiasi na kusababisha mafuriko makubwa.”​—Stefan Uhlenbrook, mkurugenzi wa masuala ya maji na hali ya hewa katika Shirika la Utabiri wa Hali ya Hewa Ulimwenguni, Julai 17, 2023.

 Je, unapata wasiwasi unaposikia ripoti hizo kuhusu hali mbaya ya hewa? Chunguza kile ambacho Biblia inasema kuhusu suala hili muhimu.

Je, hali mbaya ya hewa iliyopo duniani ilitabiriwa katika Biblia?

 Ndiyo.Viwango vya juu sana vya joto ulimwenguni na majanga mengine yanayosababishwa na hali mbaya ya hewa ni miongoni mwa matukio ambayo Biblia ilitabiri yangetukia katika siku zetu. Kwa mfano, Yesu alitabiri kwamba tungeona “mambo yenye kuogopesha” au “mambo ya kutisha.” (Luka 21:11; Union Version) Kupanda kwa kiwango cha joto ulimwenguni kumewafanya watu wengi wawe na wasiwasi kwamba wanadamu wataiharibu kabisa dunia.

Je, hali duniani zitazorota hivi kwamba viumbe-hai watashindwa kuishi humo?

 Hapana. Mungu aliumba dunia iwe makao yetu ya kudumu; hataruhusu wanadamu waiharibu dunia. (Zaburi 115:16; Mhubiri 1:4) Ukweli ni kwamba ameahidi “kuwaharibu wale wanaoiharibu dunia.”​—Ufunuo 11:18.

 Biblia inaonyesha kwamba Mungu ana uwezo na atailinda dunia isiangamizwe kutokana na majanga yanayosababishwa na hali mbaya ya hewa.

  •   “[Mungu] huituliza dhoruba ya upepo; mawimbi ya bahari hunyamaza.” (Zaburi 107:29) Mungu ana nguvu za kudhibiti hali ya hewa. Ana uwezo wa kutatua matatizo ya uharibifu wa mazingira yanayosababisha hali mbaya ya hewa inayofanya watu wateseke.

  •   “Unaitunza dunia, unaifanya izae kwa wingi na kuitajirisha sana.” (Zaburi 65:9) Kwa msaada wa Mungu dunia hii itakuwa paradiso.

 Ili ujifunze mengi zaidi kuhusu ahadi ya Biblia kwamba mazingira yatarekebishwa, ona makala yenye kichwa “Ni Nani Atakayeiokoa Dunia?