Ona video zinazopatikana

Sababu Gani Tunaishi?

Sababu Gani Tunaishi?

Jibu la Biblia

 Ulizo hilo linaweza kuulizwa kwa maneno mengine hivi: Sababu gani tuko hapa duniani? Je, Maisha yangu yana kusudi? Biblia inaonyesha kwamba kufanya urafiki pamoja na Mungu ndilo kusudi la maisha yetu. Fikiria mambo haya ya kweli ambayo Biblia inaonyesha.

  •   Mungu ni Muumbaji wetu. Biblia inasema hivi: “[Mungu] ndiye aliyetufanya, wala si sisi wenyewe.”​—Zaburi 100:3; Ufunuo 4:11.

  •   Mungu aliumba kila kitu, kutia ndani sisi akiwa na kusudi fulani.​—Isaya 45:18.

  •   Mungu alituumba na “uhitaji wa kiroho,” ambao unatia ndani tamaa ya kuwa na maisha yenye kusudi ao maana. (Mathayo 5:3) Mungu anataka tutosheleze tamaa hiyo.​—Zaburi 145:16.

  •   Tunatosheleza uhitaji wetu wa kiroho kwa kuendelea kufanya urafiki pamoja na Mungu. Hata ikiwa mutu anaweza kufikiri kwamba haiwezekani kuwa rafiki ya Mungu, Biblia inatutia moyo hivi: ‘Mukaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.’​—Yakobo 4:8; 2:23.

  •   Ili kuwa marafiki wa Mungu, tunapaswa kuishi kulingana na mapenzi yake. Biblia inazungumuzia jambo hilo kwenye Mhubiri 12:13: ‘Muheshimu Mungu, na utii amri zake, kwa maana hiyo ndiyo sababu tuliumbwa.’​—Good News Translation.

  •   Katika siku zinazokuja, tutajionea kwa ukamili sababu iliyofanya Mungu awaumbe wanadamu wakati atakapomaliza mateso yote na kuwatolea marafiki wake uzima wa milele.​—Zaburi 37:10, 11.