Ya Kwanza ya Petro 2:1-25

  • Mukomalishe tamaa kwa ajili ya neno (1-3)

  • Majiwe yenye uzima yenye yanajengwa kuwa nyumba ya kiroho (4-10)

  • Kuishi kama wageni katika ulimwengu (11, 12)

  • Kujitiisha kwenye kufaa (13-25)

    • Kristo, mufano wetu (21)

2  Basi muache ubaya wote+ na udanganyifu na unafiki na wivu na kusemana mubaya.  Kama watoto wadogo wenye wametoka kuzaliwa,+ mukomalishe tamaa kwa ajili ya maziwa yenye hayachanganywe na kitu* ya lile neno, ili kupitia hayo mukomae kufikia wokovu,+  kwa sababu mumeonja na kuona kwamba Bwana ni mwenye fazili.  Wakati munakuja kwake, jiwe lenye uzima lenye lilikataliwa na wanadamu+ lakini lenye lilichaguliwa, lenye samani kwa Mungu,+  ninyi wenyewe pia kama majiwe yenye uzima munajengwa kuwa nyumba ya kiroho+ kusudi mukuwe ukuhani mutakatifu, ili kutoa zabihu za kiroho+ zenye kukubalika kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.+  Kwa maana Andiko linasema: “Angalia! Ninaweka katika Sayuni jiwe lenye lilichaguliwa, jiwe la musingi la pembe lenye samani, na mutu yeyote mwenye anaonyesha imani katika jiwe hilo hatakata tamaa* hata kidogo.”+  Kwa hiyo, yeye ni mwenye samani kwenu, kwa sababu ninyi ni waamini; lakini kwa wale wenye hawaamini, “jiwe lenye wajenzi walikataa+ ndilo limekuwa jiwe kubwa la pembe,”*+  na “jiwe la kukwaza na mwamba wa kuangusha.”+ Wanajikwaa kwa sababu hawatii lile neno. Huo ndio mwisho wenye unawangojea.  Lakini ninyi ni “jamii yenye ilichaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu,+ watu wenye wanapaswa kuwa mali ya pekee,+ ili mutangaze kotekote sifa za muzuri zaidi”*+ za Ule mwenye aliwaita kutoka katika giza kuingia katika mwangaza wake wa ajabu.+ 10  Kwa maana wakati fulani ninyi hamukukuwa watu, lakini sasa ninyi ni watu wa Mungu;+ wakati fulani hamukukuwa mumeonyeshwa rehema, lakini sasa mumepokea rehema.+ 11  Wapendwa, ninawaomba ninyi kama wageni na wakaaji wa muda+ kwamba muendelee kujiepusha na tamaa za mwili,+ zenye zinapigana vita na ninyi.*+ 12  Muendelee kuwa na mwenendo muzuri kati ya mataifa,+ ili wakati wanawashitaki kuwa watenda-zambi, washuhudie kwa macho yao matendo yenu ya muzuri,+ na hivyo, wamutukuze Mungu katika siku ya uchunguzi wake. 13  Kwa ajili ya Bwana, mujitiishe kwa kila kitu chenye kilifanywa na mwanadamu,*+ ikuwe ni kwa mufalme+ akiwa mukubwa 14  ao kwa magavana wakiwa wametumwa naye ili kutoa azabu kwa watenda-maovu lakini kusifu wale wenye wanatenda mema.+ 15  Kwa maana ni mapenzi ya Mungu kwamba kwa kutenda mema munyamazishe* maneno ya kijinga ya watu wenye hawana akili.+ 16  Mukuwe kama watu huru,+ mukitumia uhuru wenu, hapana kama kifuniko* cha kufanya mabaya,+ lakini kama watumwa wa Mungu.+ 17  Muheshimie watu wa namna zote,+ mupende ushirika muzima wa ndugu,*+ mumuogope Mungu,+ mumuheshimie mufalme.+ 18  Watumishi wajitiishe kwa mabwana wao kwa woga wote wenye kufaa,+ haiko tu kwa wale wenye kuwa wema na wenye usawaziko, lakini pia kwa wale wenye ni nguvu kupendeza. 19  Kwa maana ni jambo lenye kupendeza wakati mutu anavumilia magumu* na kuteseka kwa njia yenye haiko ya haki kwa sababu ya zamiri kwa Mungu.+ 20  Kwa maana kuko faida gani kama wakati munapigwa kwa sababu ya kufanya zambi na munavumilia jambo hilo?+ Lakini kama munavumilia mateso kwa sababu ya kufanya mema, jambo hilo linamupendeza Mungu.+ 21  Kwa kweli, muliitwa kwenye njia hii, kwa sababu hata Kristo aliteseka kwa ajili yenu,+ akiwaachia ninyi mufano ili mufuate hatua zake kwa ukaribu.+ 22  Yeye hakufanya zambi,+ na udanganyifu haukupatikana katika kinywa chake.+ 23  Wakati alikuwa anatukanwa,+ hakujibu kwa matukano.+ Wakati alikuwa anateseka,+ hakuogopesha watu, lakini alijitia katika mikono ya Ule mwenye anahukumu+ kwa haki. 24  Yeye mwenyewe alibeba zambi zetu+ katika mwili wake mwenyewe juu ya muti,+ ili tukufe kuhusiana* na zambi na tuishi kuhusiana na haki. Na “kwa vidonda vyake muliponyeshwa.”+ 25  Kwa maana mulikuwa kama kondoo wenye kupotea njia,+ lakini sasa mumerudia kwa muchungaji+ na mwangalizi wa nafsi zenu.*

Maelezo ya Chini

Ao “safi.”
Tnn., “hatapatishwa haya.”
Tnn., “kichwa cha pembe.”
Tnn., “tabia za muzuri,” ni kusema, sifa na matendo yake yenye kustahili kusifiwa.
Ao “na nafsi.”
Ao “kila shirika la kibinadamu.”
Tnn., “mufunge vinywa.”
Ao “kisingizio.”
Tnn., “undugu.”
Ao “huzuni; maumivu.”
Ao “tuachane.”
Ao “uzima wenu.”