Kwa Waebrania 12:1-29

  • Yesu, Mukamilishaji wa imani yetu (1-3)

    • Wingu kubwa la mashahidi (1)

  • Usizarau nizamu ya Yehova (4-11)

  • Fanyia miguu yako njia zenye kunyooka (12-17)

  • Kukaribia Yerusalemu la mbinguni (18-29)

12  Hivyo basi, kwa kuwa tuko na wingu kubwa hivyo la mashahidi lenye linatuzunguka, tutupe pia kila uzito na zambi yenye kutuzuia kwa wepesi,+ na tukimbie kwa uvumilivu shindano la mbio lenye limewekwa mbele yetu,+  wakati tunakaza macho kwa uangalifu juu ya Kiongozi Mukubwa na Mukamilishaji wa imani yetu, Yesu.+ Kwa sababu ya furaha yenye iliwekwa mbele yake, alivumilia muti wa mateso,* akazarau haya, na amekaa kwenye mukono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Mungu.+  Kwa kweli, mufikirie sana ule mwenye amevumilia maneno makali kama hayo kutoka kwa watenda-zambi+ kinyume cha faida zao wenyewe, ili musichoke na kuacha.*+  Katika lile pambano lenu na zambi, hamujapambana hata kidogo kufikia hatua ya damu yenu kumwangwa.  Na mumesahau kabisa kile kitia-moyo chenye kinasema na ninyi kama wana: “Mwana wangu, usizarau nizamu kutoka kwa Yehova,* na usikate tamaa wakati anakurekebisha;  kwa maana wale wenye Yehova* anapenda anawatia nizamu, kwa kweli, anamupiga fimbo* kila mutu mwenye anapokea kama mwana.”+  Muko na lazima ya kuvumilia kama sehemu ya nizamu* yenu. Mungu anawatendea ninyi kama wana.+ Kwa maana ni mwana gani mwenye hatiwe nizamu na baba yake?+  Lakini kama ninyi wote hamujashiriki katika kupokea nizamu hii, kwa kweli ninyi ni watoto haramu, na hamuko wana.  Zaidi ya hayo, baba zetu wa kibinadamu* walikuwa wanatutia nizamu, na tuliwapatia heshima. Je, hatupaswe kujitiisha hata zaidi kwa Baba wa maisha yetu ya kiroho na kuishi?+ 10  Kwa maana walitutia nizamu kwa wakati kidogo kulingana na namna waliona kuwa inafaa, lakini yeye anafanya vile kwa faida yetu ili tushiriki utakatifu wake.+ 11  Ni kweli, hakuna nizamu yenye inaonekana kwa sasa kuwa yenye kufurahisha, lakini inaumiza;* lakini kisha, inazaa tunda lenye amani la haki kwa wale wenye wamezoezwa nayo. 12  Kwa hiyo, mutie nguvu mikono yenye inaregea na magoti yenye kuwa zaifu,+ 13  na muendelee kufanyia miguu yenu njia zenye kunyooka,+ ili kile chenye ni kilemavu kisiteguke, lakini, kiponywe. 14  Mufuatie amani pamoja na watu wote+ na utakaso*+ wenye bila huo hakuna mutu mwenye atamuona Bwana. 15  Mukuwe waangalifu kwamba mutu yeyote asikose kupata fazili zenye hazistahiliwe za Mungu, ili muzizi wowote wenye sumu usichipuke na kuleta taabu na wengi wachafuliwe nao;+ 16  na mukuwe waangalifu ili katikati yenu kusikuwe mwasherati* ao mutu yeyote mwenye haheshimie mambo matakatifu, kama vile Esau, mwenye alitoa haki zake za kuwa muzaliwa wa kwanza kwa kubadilishana na chakula kimoja.+ 17  Kwa maana munajua kwamba kisha pale, wakati alitaka kuriti baraka, alikataliwa; kwa maana, hata kama alijaribu kwa bidii kubadilisha mawazo* kwa kutoa machozi,+ hakuweza.* 18  Kwa maana hamukukaribia kitu chenye kinaweza kuguswa+ na chenye kimewashwa moto,+ na wingu jeusi na giza nzito na zoruba,+ 19  na mulio wa tarumbeta+ na sauti ya maneno+ yenye wakati watu waliyasikia, waliomba kwamba wasiambiwe neno lingine lolote.+ 20  Kwa maana hawakuweza kuvumilia amri hii: “Hata munyama akigusa mulima, anapaswa kupigwa majiwe.”+ 21  Pia, wonyesho huo ulikuwa wenye kuogopesha sana mupaka Musa akafikia kusema: “Ninaogopa na kutetemeka.”+ 22  Lakini ninyi mumekaribia Mulima Sayuni+ na muji wa Mungu mwenye kuishi, Yerusalemu la mbinguni,+ na makumi ya maelfu ya malaika 23  katika mukusanyiko mukubwa,+ na kutaniko la wazaliwa wa kwanza wenye wameandikishwa mbinguni, na Mungu Muamuzi wa watu wote,+ na maisha ya kiroho+ ya wenye haki wenye wamefanywa wakamilifu,+ 24  na Yesu mupatanishi+ wa agano jipya,+ na damu yenye ilinyunyizwa,* yenye inasema kwa njia ya muzuri zaidi kuliko damu ya Abeli.+ 25  Mufanye angalisho ili musikatae kumusikiliza* ule mwenye anasema. Kwa maana kama wale wenye walikataa kumusikiliza ule mwenye alitoa onyo la Mungu duniani hawakuponyoka, sisi hatutaponyoka hata kidogo kama tunageuka na kuacha ule mwenye anasema kutoka mbinguni!+ 26  Wakati huo sauti yake ilitikisa dunia,+ lakini sasa ameahidi: “Na mara moja tena nitatikisa hapana dunia tu lakini pia mbingu.”+ 27  Sasa maneno “na mara moja tena” yanaonyesha kuondolewa kwa vitu vyenye kutikiswa, vitu vyenye vilifanywa, ili vitu vyenye havitikiswe vibakie. 28  Kwa hiyo, kwa kuwa tutapokea Ufalme wenye hauwezi kutikiswa, tuendelee kupokea fazili zenye hazistahiliwe, zenye kupitia hizo tutamutolea Mungu utumishi mutakatifu kwa njia yenye kukubalika, kwa kumuogopa Mungu na kumuheshimia. 29  Kwa maana Mungu wetu ni moto wenye kuteke­teza.+

Maelezo ya Chini

Ao “kuzimia katika nafsi zenu.”
Ao “anapatia azabu.”
Ao “mazoezi.”
Tnn., “baba za mwili wetu.”
Ao “inahuzunisha.”
Ao “utakatifu.”
Angalia Maana ya Maneno, “Uasherati.”
Ni kusema, mawazo ya baba yake.
Tnn., “hakupata nafasi kwa ajili ya hilo.”
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Ao “musitoe visingizio kwa; musimuzarau.”