Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Juu ya Nini Batu Habaheshimiake Tena Bengine?

Juu ya Nini Batu Habaheshimiake Tena Bengine?

JUU YA NINI NI JAMBO YA MAANA KUHESHIMIA BENGINE?

Wakati tunaheshimia bengine, ile itasaidia hali ya mubaya isiharibike zaidi.

  • Mezali moya ya Biblia inasema hivi: “Jibu la upole linatuliza kasirani kali, lakini neno la ukali linachochea hasira.” (Mezali 15:1) Maneno na matendo ya kukosa heshima inaletaka tu matokeo ya mubaya, iko sawa vile kumwanga mafuta ku moto.

  • Yesu alisema: “Kinywa kinasema mambo yenye kujaa katika moyo.” (Matayo 12:34) Wakati hatuheshimie bengine, ile inaweza kuonyesha vile tunaonaka batu ya rangi ya ngozi yenye kuwa tofauti na yetu, benye kuwa na kabila tofauti na yetu, batu ya inchi tofauti na yetu, ao batu benye kuwa na hali ya maisha yenye kuwa tofauti na yetu.

    Mu uchunguzi wenye ulifanywa hivi karibuni mu inchi 28, zaidi ya batu 32000 baliulizwa maulizo. Na zaidi ya nusu (65%) kati ya bale batu balisema kama, leo batu mingi biko naendelea tu kuwa na tabia ya kukosa heshima mu njia yenye habayaonaka.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

Ikuwe uko ku masomo ao ku kazi, uheshimie batu yote hata kama habana mawazo sawa yako. Ujikaze kujua ni mu mambo gani njo munawaza mu njia moya. Ile itakusaidia usikuwe nasema bengine mubaya ao kubahukumu.

“Muache kuhukumu ili musihukumiwe.”—Matayo 7:1.

Utendee bengine vile unapendaka bakutendee. Kama unatendeaka bengine muzuri, ile inaweza kubachochea nabo bakutendee muzuri.

“Kama vile munataka watu wawatendee ninyi, muwatendee kwa njia ileile.”—Luka 6:31.

Ukuwe mwenye kusamehe. Utumainie kama pengine mutu mwenye alikusema ao kukutendea mubaya hakufanya vile kwa kupenda, njo maana uachilie tu ile mambo.

“Ufahamu wa mutu hakika unatuliza kasirani yake, na ni uzuri kwake kuachilia kosa.”—Mezali 19:11.

MAMBO YENYE TUKO NAFANYA

Mashahidi wa Yehova wanajikazaka kuheshimia bengine fasi kwenye banaishi ao kwenye banatumikaka na banasaidiaka bengine kufanya vile.

Tunafundishaka Biblia kwa bure, lakini hatubakazake imani yetu ao mawazo yetu. Kuliko kufanya vile, tunajikazaka kutumikisha mashauri ya Biblia kwa kuambia bengine ujumbe wetu “kwa upole na heshima kubwa.”—1 Petro 3:15; 2 Timoteo 2:24.

Hatukuwake na ubaguzi njo maana tunakaribishaka ku mikutano yetu batu ya desturi mbalimbali benye banapenda kujifunza mambo yenye Biblia inafundisha. Tunajikazaka ‘kuheshimia watu wa namna zote,’hata kama hatukubaliane na maamuzi yenye banakamata—1 Petro 2:17.

Tunaheshimia mamlaka ya serikali ya kwenye tunaishi. (Waroma 13:1) Tunatii sheria na tulipa kodi ao taxe. Na hata kama hatujiingizake mu mambo ya politike, tunaheshimia haki ya bengine ya kujikamatia maamuzi mu mambo ya politike.