Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Muamuzi wa Dunia Yote’ Anafanya Sikuzote Mambo Yenye Kuwa Sawa

‘Muamuzi wa Dunia Yote’ Anafanya Sikuzote Mambo Yenye Kuwa Sawa

“Yeye Mwamba, kazi zake ni kamilifu, kwa maana njia zake zote ni haki.”—KUMBUKUMBU LA TORATI 32:4.

NYIMBO: 112, 89

1. Namna gani Abrahamu alionyesha kuwa alitumainia haki ya Yehova? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

‘JE, MUAMUZI wa dunia yote hatafanya lililo sawa?’ (Mwanzo 18:25) Mwanaume muaminifu Abrahamu hakuuliza ulizo hilo kwa sababu alikuwa na mashaka. Lakini, ulizo lake lilionyesha kuwa alikuwa hakika kama Yehova angehukumu miji ya Sodoma na Gomora kwa haki kamilifu. Alikuwa hakika kama Yehova hangeweza hata kidogo ‘kuua mutu muadilifu pamoja na muovu.’ Hilo lilikuwa jambo lisilowaziwa kwa Abrahamu. Kisha, Yehova alisema juu yake mwenyewe hivi: ‘Mwamba, kazi zake ni kamilifu, kwa maana njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, ambaye hana ukosefu wowote wa haki; Yeye ni muadilifu na munyoofu.’—Kumbukumbu la Torati 31:19; 32:4.

2. Sababu gani Yehova hawezi kutenda bila haki hata kidogo?

2 Sababu gani Abrahamu alikuwa hakika kuwa Yehova angefanya sikuzote mambo yenye kuwa sawa? Kwa sababu Yehova ndiye mufano mukubwa zaidi wa haki na uadilifu. Kwa kweli, maneno “haki” na “uadilifu” yanatumiwa mara nyingi pamoja katika Maandiko ya Kiebrania kwa sababu yako na maana moja. Kwa hiyo, kwa sababu kanuni za Yehova ni za haki sikuzote, hukumu yake itakuwa sawa sikuzote. Biblia inasema hivi: “Anapenda uadilifu na haki.”—Zaburi 33:5.

3. Toa mufano fulani wa ukosefu wa haki wenye kuwa katika ulimwengu leo.

3 Ni jambo lenye kutia moyo kujua kama Yehova anatenda kwa haki sikuzote. Lakini leo, ulimwengu unajaa ukosefu wa haki. Kwa mufano, watu wamehukumiwa na kufungwa katika gereza kwa sababu ya makosa yenye hawakufanya. Kisha kupata ushuhuda mupya wenye kuhakikisha kuwa hawakufanya makosa, watu fulani wamefikia kuachiliwa, lakini walikuwa tayari wamepitisha miaka mingi katika gereza. Ukosefu wa haki wa namna hiyo unaleta huzuni na hasira. Lakini, kuko aina ingine ya ukosefu wa haki yenye inaweza kuwa hata vigumu sana kuvumilia. Ni aina gani hiyo ya ukosefu wa haki?

UKOSEFU WA HAKI NDANI YA KUTANIKO

4. Namna gani imani ya Mukristo inaweza kujaribiwa?

4 Wakristo wanajua kama wanaweza kutendewa bila haki inje ya kutaniko la Kikristo. Lakini, imani yetu inaweza kujaribiwa ikiwa tunaona ao tunatendewa ndani ya kutaniko jambo fulani lenye kuonekana kuwa ni ukosefu wa haki. Ikiwa hilo linatokea, utatenda namna gani? Utaacha jambo hilo likukwaze?

5. Sababu gani Mukristo hapaswe kushangaa ikiwa anaona ukosefu wa haki katika kutaniko ao anatendewa hivyo?

5 Kwa sababu sisi wote hatukamilike na tunafanya makosa, tunajua kwamba inawezekana mutu fulani atutendee bila haki ao sisi tutendee mutu mwengine bila haki katika kutaniko. (1 Yohana 1:8) Hata kama jambo hilo halitokee mara nyingi, Wakristo waaminifu hawashangae ao kukwazika wakati jambo fulani la ukosefu wa haki linatokea. Ndiyo sababu Yehova ametupatia mashauri ya muzuri katika Neno lake ili yatusaidie tubakie washikamanifu hata wakati Wakristo wenzetu wanatutendea mubaya.​—Zaburi 55:12-14.

6, 7. Namna gani ndugu mumoja alitendewa bila haki katika kutaniko, na ni sifa gani zilimusaidia?

6 Fikiria mufano wa Willi Diehl. Kuanzia mwaka wa 1931, Ndugu Diehl alitumikia kwa uaminifu kwenye Beteli ya Bern, Uswisi. Katika mwaka wa 1946, alisoma darasa la 8 la Masomo ya Gileadi katika New York, Amerika. Kisha kumaliza masomo, alifikia kupewa mugawo wa kutumika katika kazi ya muzunguko katika Uswisi. Katika habari juu ya maisha yake, Ndugu Diehl alisema hivi: “Katika Mwezi wa 5, 1949, nilijulisha tawi ya Bern ya kwamba nilikuwa ninapanga kuoa.” Ndugu wa makao makubwa ya Bern walijibu namna gani? Ndugu Diehl aliendelea kueleza hivi: “Waliondoa madaraka yangu yote, wakaniachia upainia tu. Sikuruhusiwa kutoa hotuba . . . Ndugu na dada wengi hawakutusalimia tena, na walitutendea kama watengwa.”

7 Ndugu Diehl alitenda namna gani? Alisema hivi: “Tulijua kama Maandiko hayakataze kufunga ndoa; kwa hiyo, tulisali sana kwa Yehova na kumutumainia.” Hata kama ndugu fulani hawakuelewa mawazo ya Yehova juu ya ndoa, kisha wakati fulani walisaidiwa kubadilisha mawazo yao, na Ndugu Diehl akarudishiwa madaraka yake. Yehova alibariki ushikamanifu wake. * (Soma maelezo ya chini.) Tunaweza kujiuliza basi hivi: ‘Ikiwa ninatendewa bila haki kwa njia hiyo, nitaonyesha uvumilivu na kungojea Yehova atengeneze mambo? Ao nitajitegemea mimi mwenyewe na kujaribu kupiganisha ukosefu huo wa haki?’—Methali 11:2; soma Mika 7:7.

8. Sababu gani tunaweza kujidanganya kwa kufikiri kama sisi ao wengine tumetendewa bila haki?

8 Ikiwa unafikiri kwamba jambo fulani la ukosefu wa haki limetendeka katika kutaniko, kumbuka kwamba pengine unajidanganya. Sababu gani? Hatukamilike na pengine tulielewa mambo mubaya. Pia pengine hatujue mambo yote. Lakini iwe tunaelewa hali fulani muzuri ao hapana, tunapaswa kusali kwa Yehova juu ya hali hiyo, kumutegemea, na kubakia washikamanifu. Kufanya hivyo kutatuzuia kuwa na ‘gazabu [hasira] juu ya Yehova.’—Soma Methali 19:3.

9. Katika habari hii na habari yenye kufuata, tutazungumuzia mifano gani?

9 Tuone mambo yenye tunaweza kujifunza kwa kuchunguza mifano tatu ya watu wa Yehova wenye walitendewa bila haki wakati wa zamani. Katika habari hii, tutazungumuzia mufano wa Yosefu wa kizazi cha Abrahamu na mambo yenye ndugu zake walimutendea. Katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia namna Yehova alitendea Mufalme Ahabu na namna mutume Petro alitenda wakati alikuwa katika Antiokia ya Siria. Wakati tunaendelea kuzungumuzia mifano hiyo, tambua njia mbalimbali za kukusaidia uendelee kushikamana na Yehova na kulinda urafiki wako pamoja naye, zaidi sana wakati unafikiri kama umetendewa bila haki.

YOSEFU ALITENDEWA BILA HAKI

10, 11. (a) Namna gani Yosefu alitendewa bila haki? (b) Wakati Yosefu alikuwa katika gereza, alipata nafasi gani?

10 Yosefu alikuwa mutumishi muaminifu wa Yehova mwenye alitendewa bila haki na watu wenye hajue. Lakini jambo lenye lilimuumiza sana ni ukosefu wa haki wenye ndugu zake mwenyewe walimutendea. Wakati Yosefu alikuwa na 17, ndugu zake walimuchukua kwa nguvu na kumuuzisha ili akuwe mutumwa. Kisha alipelekwa Misri. (Mwanzo 37:23-28; 42:21) Kisha, wakati Yosefu alikuwa katika Misri, alishitakiwa mambo ya uongo kwamba alijaribu kulala kinguvu mwanamuke fulani na akafungwa katika gereza bila kusamba. (Mwanzo 39:17-20) Yosefu aliteseka kama mutumwa na mufungwa kwa miaka 13 hivi. Mufano wa Yosefu unaweza kutufundisha mambo gani yenye yanaweza kutusaidia wakati ndugu ao dada zetu wanatutendea bila haki?

11 Wakati Yosefu alikuwa katika gereza, mukubwa wa watumishi wa kumupatia mufalme kinywaji alifungwa pia katika gereza. Usiku moja, mutumishi huyo aliota ndoto, na Yehova alisaidia Yosefu kufasiria ndoto hiyo. Yosefu alifasiria kuwa mutumishi huyo angefunguliwa kutoka katika gereza na angemutumikia tena Farao. Kisha Yosefu akachukua nafasi hiyo ili kufasiria mwanaume huyo hali yake. Mambo yenye Yosefu alisema na ile yenye hakusema yanaweza kutufundisha mambo mengi.​—Mwanzo 40:5-13.

12, 13. (a) Tunajua namna gani kwamba Yosefu hakukubali tu ukosefu wa haki? (b) Ni mambo gani yenye Yosefu hakumuambia mutumishi wa kumupatia mufalme kinywaji?

12 Soma Mwanzo 40:14, 15. Ona kwamba Yosefu alisema kuwa ‘ametekwa nyara [kuchukuliwa kwa nguvu].’ Neno lenye Biblia inatumia hapa linaweza pia kumaanisha “kuibwa.” Kwa kweli, alitendewa bila haki. Pia Yosefu alisema waziwazi kama anashitakiwa juu ya kosa lenye hakufanya. Ndiyo sababu alimuomba mutumishi huyo wa mufalme, amusemee kwa Farao. Yosefu alikuwa na kusudi gani? Alisema hivi: ‘[Ili] nitoke inje ya nyumba hii.’

13 Yosefu alikubali tu hali yake bila kujikaza kufanya jambo fulani juu ya hali hiyo? Hapana! Yosefu alijua kama alitendewa mambo mengi bila haki. Ndiyo sababu alimuelezea mutumishi huyo hali yake, na kutumaini kama mwanaume huyo angemusaidia. Lakini ona kwamba Maandiko hayaseme kama Yosefu aliambia mutu yeyote ao hata Farao, kama ndugu zake ndio walimuchukua kwa nguvu. Kwa kweli, wakati ndugu za Yosefu walifika Misri na kufanya amani pamoja naye, Farao aliwakaribisha ili waishi katika Misri na kufurahia ‘wema wa inchi yote.’—Mwanzo 45:16-20.

Kusema-sema mubaya kunaweza kufanya hali ikuwe mubaya zaidi (Picha hizi zinapatana na fungu la 14)

14. Ni nini itatuzuia kusema jambo fulani lenye kuumiza ikiwa tunatendewa bila haki katika kutaniko?

14 Ikiwa tunafikiri kuwa tumetendewa bila haki katika kutaniko, tunapaswa kuwa waangalifu ili tusiseme-seme mubaya juu ya hali hiyo. Kwa kweli, tunapaswa kuomba wazee musaada na kuwaambia ikiwa ndugu ao dada fulani amefanya zambi fulani nzito. (Mambo ya Walawi 5:1) Lakini, katika hali nyingi zenye hazihusu zambi nzito, tunaweza kufanya amani pamoja na ndugu ao dada bila kuambia mutu yeyote, ao hata wazee. (Soma Mathayo 5:23, 24; 18:15.) Tuendelee basi kuwa washikamanifu na kutumia kanuni za Biblia katika hali hizo. Wakati fulani tunaweza kutambua kama hatukuelewa muzuri hali fulani na kama hatukutendewa bila haki hata kidogo. Kisha tutafurahi kwa sababu hatukufanya hali hiyo ikuwe mubaya zaidi kwa kusema mambo ya mubaya juu ya ndugu ao dada yetu! Kumbuka kwamba iwe tuko na haki ao hapana, kusema jambo fulani lenye kuumiza hakuwezi kutengeneza mambo hata kidogo. Ushikamanifu kwa Yehova na kwa ndugu na dada zetu utatuzuia kufanya kosa kama hilo. Muandikaji mumoja wa zaburi alisema kama kuko mutu “anayetembea bila kosa.” Mutu huyo ‘hakuchongea kwa ulimi wake. Hakumufanyia mwenzake jambo lolote baya.’—Zaburi 15:2, 3; Yakobo 3:5.

KUMBUKA URAFIKI WAKO WA MAANA ZAIDI

15. Namna gani urafiki wa Yosefu pamoja na Yehova ulikuwa baraka kwake?

15 Mufano wa Yosefu unaweza kutufundisha jambo lingine la maana. Kwa miaka 13 yenye alitendewa bila haki, Yosefu alionyesha kwamba aliona mambo namna Yehova alikuwa anayaona. (Mwanzo 45: 5-8) Hakumulaumu Yehova hata kidogo juu ya hali yake. Kwa kweli, Yosefu hakusahau namna alitendewa bila haki, lakini hakuweka kinyongo. Na jambo la maana zaidi ni kwamba, hakuruhusu makosa na matendo ya mubaya ya wengine yamutenganishe na Yehova. Ushikamanifu wa Yosefu ulimupatia nafasi ya kuona namna Yehova anatengeneza mambo na kumubariki yeye na familia yake.

16. Sababu gani tunapaswa kumukaribia Yehova hata zaidi ikiwa tunatendewa bila haki katika kutaniko?

16 Vilevile, sisi pia tunapaswa kupenda sana na kulinda urafiki wetu pamoja na Yehova. Hatupaswe hata kidogo kuruhusu makosa ya ndugu na dada zetu yatutenganishe na Mungu mwenye tunapenda na kuabudu. (Waroma 8:38, 39) Lakini, ikiwa tunatendewa bila haki katika kutaniko, tuige basi mufano wa Yosefu na tumukaribie Yehova hata zaidi. Ujikaze kuona mambo namna anayaona. Kisha kufanya yetu yote ili kumaliza tatizo kwa kufuata kanuni za Biblia, tunapaswa kuacha mambo katika mikono ya Yehova. Tunaweza kuwa hakika kama atatengeneza mambo katika njia yake mwenyewe na kwa wakati wake.

TUMAINIA ‘MUAMUZI WA DUNIA YOTE’

17. Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunatumainia ‘muamuzi wa dunia yote’?

17 Wakati tunaendelea kuishi katika ulimwengu huu muovu, tunaweza kutazamia kwamba tutatendewa bila haki. Mara chache sana, wewe ao mutu mwengine mwenye unajua anaweza kuona ao kutendewa katika kutaniko jambo fulani lenye kuonekana kuwa la ukosefu wa haki. Usikwazike. (Zaburi 119:165) Lakini, uendelee kuwa mushikamanifu kwa Mungu, usali kwake na kumuomba musaada, na umutegemee. Kumbuka kwamba kwa sababu ya kukosa kukamilika pengine ulielewa mambo mubaya, na pengine haujue mambo yote. Uige mufano wa Yosefu na uepuke kusema mubaya, kwa sababu hilo linaweza kufanya hali ikuwe ya mubaya zaidi. Mwishowe, kuliko kujitegemea wewe mwenyewe, uazimie kubakia mushikamanifu na kungojea Yehova kwa uvumilivu ili atengeneze mambo. Ukifanya hivyo, Yehova atakukubali na kukubariki kama vile alitendea Yosefu. Unaweza kuwa hakika kama Yehova, ‘muamuzi wa dunia yote,’ atafanya mambo yenye kuwa sawa sikuzote, “kwa maana njia zake zote ni haki.”—Mwanzo 18:25; Kumbukumbu la Torati 32:4.

18. Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

18 Katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia mifano mingine mbili ya ukosefu wa haki kati ya watu wa Yehova wa wakati wa zamani. Mifano hiyo itatusaidia kuona namna sifa ya unyenyekevu na ya kusamehe zitatusaidia kufuata kanuni za Yehova juu ya haki.

^ fu. 7 Soma habari juu ya maisha ya Willi Diehl, “Yehova Ni Mungu Wangu Nitakayemtumaini,” katika gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 11, 1991.