Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Musa—Mwanaume Aliyeonyesha Upendo

Musa—Mwanaume Aliyeonyesha Upendo

UPENDO NI NINI? Upendo ni sifa ya kupendezwa sana na watu wengine. Mutu mwenye upendo anaonyesha kwa maneno na matendo yake namna anavyojisikia juu ya wale ambao anapenda, hata ikiwa hilo litamuomba ajinyime mwenyewe mambo fulani.

 

MUSA ALIONYESHA UPENDO NAMNA GANI? Musa alionyesha kuwa alimupenda Mungu. Katika njia gani? Kumbuka maneno haya ya andiko la 1 Yohana 5:3: ‘Kumupenda Mungu kunamaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake.’ Musa aliishi kulingana na kanuni hiyo. Alitii mambo yote ambayo Mungu alimuomba kufanya, kama vile mugawo mugumu wa kusimama mbele ya Farao mwenye nguvu, na mugawo ulioonekana kuwa mwepesi zaidi wa kupiga fimbo yake juu ya Bahari Nyekundu. Iwe amri aliyopewa ilikuwa nyepesi ao ngumu kutimiza, Musa alitii. “Alifanya vivyo hivyo.”​—Kutoka 40:16.

 

Musa alionyesha kuwa aliwapenda Waisraeli wenzake. Waisraeli walitambua kwamba Yehova alikuwa anamutumia Musa ili kuongoza watu wake, kwa hiyo, walimuendea Musa ili kumuelezea magumu yao mbalimbali. Tunasoma hivi: ‘Watu wakasimama mbele ya Musa tangu asubuhi mupaka jioni.’ (Kutoka 18:13-16) Wazia namna Musa alivyochoka sana kwa sababu ya kuwasikiliza Waisraeli waliokuja kumuelezea magumu yao tangu asubuhi mupaka mangaribi! Lakini, Musa alifurahi kuwasaidia Waisraeli kwa sababu aliwapenda.

Zaidi ya kuwasikiliza, Musa alisali pia kwa ajili ya watu hao ambao alipenda. Alisali hata kwa ajili ya wale waliomutendea vibaya! Kwa mufano, wakati Miriamu, dada ya Musa, alimunungunikia Musa, Yehova alimupiga Miriamu kwa ugonjwa wa ukoma. Kuliko kufurahia azabu hiyo, Musa alimusihi Mungu kwa ajili ya Miriamu kwa kusali hivi: ‘Ee Mungu, tafazali! Muponye, tafazali!’ (Hesabu 12:13) Ni upendo tu ndio ulimuchochea Musa kutoa sala hiyo isiyo na uchoyo kwa ajili ya dada yake.

TUNAWEZA KUJIFUNZA NINI JUU YA UPENDO WA MUSA? Tunaweza kumuiga Musa kwa kuonyesha upendo mwingi kwa Mungu. Upendo kama huo unatuchochea kutii amri zake “kutoka moyoni.” (Waroma 6:17) Tunapotii amri za Mungu kutoka moyoni, tunafurahisha moyo wake. (Methali 27:11) Na pia tunafaidika sisi wenyewe. Na zaidi ya yote, tunapomutumikia Mungu kwa sababu ya kuchochewa na upendo wa kweli, tutafanya si mambo yaliyo sawa tu lakini pia tutayafanya kwa moyo wenye furaha!​—Zaburi 100:2.

 

Njia nyingine ya kumuiga Musa ni kukomalisha upendo wa kujitoa kwa ajili ya wengine. Wakati marafiki ao watu wa familia wanapokuja kutuelezea mahangaiko yao, upendo unatuchochea (1) kuwasikiliza kwa moyo wote; (2) kuelewa hali yao, ao kujisikia moyoni kama wanavyojisikia; na (3) kuwaelezea kwamba tunawahangaikia.

Kama Musa, tunaweza kusali kwa ajili ya watu ambao tunapenda. Wakati fulani, tunaweza kujisikia kwamba hatuna uwezo wa kuwasaidia wanapotuelezea magumu yao. Tunaweza hata kusema, “Pole sana, sina jambo la kufanya isipokuwa tu kusali kwa ajili yako.” Lakini kumbuka hili: “Sala ya mtu mwema ina nguvu ya kutenda mengi.” (Yakobo 5:16, Biblia Habari Njema) Sala zetu zinaweza kabisa kumuchochea Yehova afanye jambo ambalo hangefanya kwa ajili ya mutu fulani. Hivyo basi, ni jambo gani nzuri zaidi tunaloweza kufanya kwa ajili ya watu tunaopenda isipokuwa tu kusali kwa ajili yao? *

Je, hauone kwamba mufano wa Musa unaweza kutufundisha mambo mengi? Hata ikiwa alikuwa mutu wa kawaida, alituachia mufano muzuri sana wa imani, unyenyekevu, na upendo. Kwa kadiri tunavyojikaza sana kuiga mufano wake, ndivyo tutafaidika sisi wenyewe na pia kuwafaidi watu wengine.​—Waroma 15:4.

^ Ili Mungu asikilize sala zetu, tunapaswa kujikaza kwa moyo wetu wote kutimiza mambo anayotuomba tufanye. Ili kupata habari zingine, soma sura ya 17 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.