Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UMUKARIBIE MUNGU

“Ni Amri Gani Iliyo ya Kwanza Kati ya Zote?”

“Ni Amri Gani Iliyo ya Kwanza Kati ya Zote?”

Tunapaswa kufanya nini ili kumupendeza Mungu? Je, ana sheria nyingi sana ambazo tunapaswa kufuata? Inapendeza kujua kwamba jibu ni hapana. Kulingana na Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, Mungu hatuombe mambo mengi.​—Soma Marko 12:28-31.

Ona kwanza mistari inayozunguka maneno hayo ya Yesu. Alikuwa anafundisha katika hekalu tarehe 11 Mwezi wa Nisani, siku chache mbele ya kifo chake. Maadui wake walijaribu kumuuliza maulizo yenye kutokeza mabishano, kwa sababu walitaka kumusukuma akosee. Kila mara, aliwanyamazisha kupitia majibu yake. Kisha, Yesu aliulizwa ulizo hili: “Ni amri gani iliyo ya kwanza kati ya zote?”​—Mustari wa 28.

Hilo lilikuwa ulizo ngumu. Wayahudi fulani walibishana kwa kupenda kujua ni sheria gani iliyokuwa ya kwanza ao ya maana zaidi kati ya sheria zaidi ya 600 ambazo zilifanyiza Sheria ya Musa. Inaonekana wengine walisema kwamba sheria zote zilikuwa na maana sawasawa na kwamba lilikuwa kosa kufikiri kuwa sheria fulani zilikuwa za maana zaidi kuliko zingine. Yesu angetoa jibu gani kwa ulizo hilo?

Katika jibu lake, Yesu hakutaja tu amri moja lakini alitaja amri mbili. Kwanza, alisema hivi: ‘Nawe lazima umupende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote.’ (Mustari wa 30; Kumbukumbu la Torati 6:5) Maneno “moyo,” “akili,” “nafsi,” na “nguvu” yanaweza kumaanisha jambo moja. * Maana ya maneno hayo ni: Tunapaswa kumupenda Yehova kwa utu wetu wote wa ndani, kwa uwezo wetu wote na mali zetu zote. Kitabu kimoja kinachofasiria Biblia kinasema hivi kuhusu maneno hayo: “Tunapaswa kumupenda Mungu kabisa.” Kwa hiyo, ikiwa unamupenda Mungu utafanya yote unayoweza ili kuishi kila siku kwa njia inayomupendeza.​—1 Yohana 5:3.

Pili, alisema hivi: ‘Mupende mwenzako kama wewe mwenyewe.’ (Mustari wa 31; Mambo ya Walawi 19:18) Kwa kweli, kuna uhusiano kati ya kumupenda Mungu na kumupenda jirani. Tunamupenda jirani yetu kwa sababu tunamupenda kwanza Mungu. (1 Yohana 4:20, 21) Ikiwa tunapenda majirani wetu kama sisi wenyewe, tutawatendea namna tunavyotaka watutendee. (Mathayo 7:12) Tukifanya hivyo, tutaonyesha kwamba tunamupenda Mungu aliyetuumba kwa mufano wake, sisi na majirani wetu.​—Mwanzo 1:26.

Yehova hawaombe waabudu wake mambo mengi, jambo ambalo anawaomba tu ni: upendo

Amri ya kumupenda Mungu na jirani ni ya maana kadiri gani? Yesu alisema hivi: “Hakuna amri nyingine yoyote iliyo kubwa zaidi kuliko hizi.” (Mustari wa 31) Katika Injili ya Mathayo, Yesu alisema kama amri zingine zote zinategemea hizo amri mbili.​—Mathayo 22:40.

Kumupenda Mungu si jambo ngumu. Mungu hatuombe mambo mengi, jambo ambalo anatuomba tu ni: upendo. Sikuzote Mungu ametaka, na ataendelea kutaka, watumishi wake wa kweli wamupende. Lakini upendo haumaanishe tu maneno ao namna mutu anavyojisikia moyoni juu ya mutu mwengine. Upendo unaonyeshwa kupitia matendo. (1 Yohana 3:18) Sababu gani usijifunze namna unavyoweza kukomalisha na kuonyesha upendo wako kwa Yehova, Mungu ambaye “ni upendo”?​—1 Yohana 4:8.

Tafazali, mwezi huu wa 3, soma Maandiko haya katika Biblia

Marko sura ya 9-16 mupaka Luka sura ya 1-6

^ Katika Biblia, neno “nafsi” linamaanisha mutu wote muzima. Kwa hiyo, neno “nafsi” linaweza kutia ndani “moyo,” “akili,” na “nguvu.”