Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kuna Tumaini Gani kwa Ajili ya Mababu Zangu?

Kuna Tumaini Gani kwa Ajili ya Mababu Zangu?

WAKATI fulani uliopita, kichwa cha habari chenye kuvutia kilitolewa katika gazeti fulani la Korea. (The Chosun Ilbo) Kichwa cha habari hiyo kiliuliza hivi: “‘Shim Cheong, Mutu Muzuri Sana,’ Mwenye Hakujua Kitu Chochote Juu ya Yesu—Alienda Katika Moto wa Mateso?”

Kichwa hicho cha habari kilichokoza watu kwa sababu Shim Cheong ni mwanamuke mwenye anapendwa sana katika hadisi ya Korea, alitoa uzima wake ili kumusaidia baba yake aliyekuwa kipofu. Alisifiwa sana kwa miaka mingi. Kwa kweli, katika inchi ya Korea, Shim Cheong amefikia kuonwa kuwa mufano muzuri wa kijana mwanamuke aliyejitoa.

Kwa watu wengi, wazo la kwamba mutu kama huyo angeazibiwa katika moto wa mateso kwa sababu hakubatizwa na kuwa Mukristo lilionekana kuwa si la haki ao hata lenye kuchukiza. Kwa vyovyote, inawaziwa kuwa jambo hilo lilitukia mbele habari juu ya Kristo iingie katika kijiji chao.

Ndani ya habari hiyo kulikuwa sehemu ya kumuuliza maulizo kiongozi wa kidini. Walimuuliza ikiwa watu wote waliokufa bila kupata nafasi ya kujifunza juu ya Yesu wamehukumiwa katika moto wa mateso. Alijibu namna gani? “Hatujue. Tunawazia tu kwamba Mungu anapaswa kuwa na kusudi fulani [kwa ajili ya watu kama hao].”

JAMBO LINALOOMBWA ILI KUPATA WOKOVU

Kitabu kimoja kinasema hivi: “Ubatizo ni wa maana ili kupata wokovu. Kama Kristo mwenyewe alivyosema, mutu asipozaliwa kwa maji na Roho Takatifu, hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu (Yoh 3.5).” (The New Catholic Encyclopedia) Kwa sababu ya maneno hayo, watu fulani wanaamini kwamba wale waliokufa bila kubatizwa wametupwa katika moto wa mateso ao kwamba wanateseka kwa njia nyingine kisha kufa kwao.

Hata hivyo, kuna watu wengine wengi wenye wanaona imani hiyo kuwa ya kipumbavu. Mamilioni ya watu walikufa bila kujua mambo Biblia inasema. Je, hilo linamaanisha kwamba wanastahili kuteseka milele? Biblia inasema nini juu ya jambo hilo?

TUMAINI LILILOAHIDIWA KATIKA BIBLIA

Biblia inaonyesha waziwazi kwamba Mungu hawazarau watu walioishi bila kujua mapenzi yake. Andiko la Matendo 17:30 linatuhakikishia kwamba “Mungu ameachilia mbali nyakati hizo za kutojua.” Sasa, Biblia inasema kuna tumaini gani kuhusu watu wanaokufa bila kupata nafasi ya kujifunza juu ya Mungu?

Ahadi ya Yesu “utakuwa pamoja nami katika Paradiso,” inamaanisha nini?

Jibu linaweza kupatikana katika maneno yenye Yesu alimuambia mutenda maovu mumoja kati ya watenda maovu wawili waliouawa pembeni yake. Mwanaume huyo alimuambia Yesu hivi: “Unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.” Yesu alimujibu namna gani? “Kwa kweli mimi nakuambia leo, utakuwa pamoja nami katika Paradiso.”—Luka 23:39-43.

Yesu aliahidi mwanaume huyo kwamba ataenda mbinguni? Hapana. Mwanaume huyo hakuwa ‘amezaliwa tena’ kupitia maji na roho, jambo lenye lilihitajiwa ili kuingia katika Ufalme wa mbinguni. (Yohana 3:3-6) Lakini, Yesu alimuahidi mutenda maovu huyo kwamba ataishi tena, katika Paradiso. Kwa kuwa mwanaume huyo alikuwa Muyahudi, inawezekana alikuwa anajua mambo fulani juu ya Paradiso duniani, ni kusema, bustani ya Edeni, inayoelezwa katika kitabu cha kwanza cha Biblia. (Mwanzo 2:8) Ahadi ya Yesu ilimuhakikishia kwamba atafufuliwa katika Paradiso wakati itarudishwa duniani.

Kwa kweli, Biblia inaahidi “ufufuo wa waadilifu [ao wenye haki] na wasio waadilifu [ao wasio haki] pia.” (Matendo 24:15) “Wasio waadilifu” ni watu wenye hawakuishi kulingana na kanuni za Mungu za haki kwa sababu hawakujua mapenzi ya Mungu. Yesu atamufufua mutenda maovu huyo asiye muadilifu aliyezungumuza naye, na pia mamilioni, pengine hata mamiliare, ya watu wengine waliokufa bila kujua mapenzi ya Mungu. Kisha, katika Paradiso duniani, watafundishwa mambo Mungu anataka wafanye, na watapata nafasi ya kuonyesha kwamba wanamupenda Mungu kwa kutii amri zake.

 WAKATI WASIO WAADILIFU WATAFUFULIWA

Wakati wasio waadilifu watafufuliwa, je, watahukumiwa kwa musingi wa matendo yao ya zamani? Hapana. Andiko la Waroma 6:7 linasema hivi: ‘Yeye ambaye amekufa ameondolewa hatia ya zambi yake.’ Wasio waadilifu wanapokufa, wanalipa zambi zao. Kwa hiyo, watahukumiwa juu ya mambo watafanya kisha kufufuliwa kwao, wala si juu ya mambo yenye walifanya bila kujua kama ni mabaya mbele wakufe. Watafaidika namna gani?

Kisha kufufuliwa, wasio waadilifu watapata nafasi ya kujifunza sheria za Mungu, zenye zitafunuliwa wakati vitabu vya kukunjwa vya mufano vitafunguliwa. Kisha hapo, watahukumiwa “kulingana na matendo yao,” ni kusema, ikiwa watamutii Mungu ao hapana. (Ufunuo 20:12, 13)Kwa wengi kati ya wale wasio waadilifu, hiyo haitakuwa nafasi ya pili, lakini itakuwa nafasi yao ya kwanza kabisa ya kuishi milele katika dunia kwa kujifunza na kufanya mapenzi ya Mungu.

Fundisho hilo la Biblia limesaidia watu wengi wamuamini tena Mungu. Yeong Sug alikuwa mumoja kati ya watu hao. Alikomaa akiwa Mukatoliki mwenye bidii. Watu fulani katika familia yake walikuwa mapadri. Kwa kuwa alitaka awe mutawa mwanamuke, alienda kuishi kwenye makao ya watawa. Baadaye, kisha kuona mambo yaliyokuwa yakifanywa huko, alivunjika moyo na akaondoka kwenye makao hayo. Zaidi ya hayo, hangekubali fundisho la moto wa mateso kwa sababu aliona kwamba kutesa watu katika moto huo hakuonyeshe haki na upendo.

Kisha, Shahidi mumoja wa Yehova alimuonyesha Yeong Sug maneno haya ya Biblia: ‘Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajue lolote kamwe, wala hawana malipo tena.’ (Mhubiri 9:5) Shahidi huyo alimusaidia atambue kwamba mababu zake hawateswe katika moto wa mateso. Lakini, wanalala katika kifo, wakingojea ufufuo.

Kwa kuwa Yeong Sug alijua kwamba watu wengi hawajasikia kweli ya Biblia, alichukua kwa uzito maneno ya Yesu yanayopatikana katika andiko la Mathayo 24:14. Andiko hilo linasema hivi: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” Leo, Yeong Sug anafanya pia kazi ya kuhubiri habari njema na anazungumuzia watu wengine tumaini lake nzuri linalotegemea Biblia.

“MUNGU HANA UBAGUZI”

Biblia inatuambia hivi: ‘Mungu hana ubaguzi, [lakini] katika kila taifa mutu ambaye anamuogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.’ (Matendo 10:34, 35) Hii ni haki kamilifu, na kila mumoja wetu anatazamia Mungu awe nayo, kwa kuwa “anapenda uadilifu na haki.”—Zaburi 33:5.