Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA

Mungu Anaona Vita Namna Gani?

Mungu Anaona Vita Namna Gani?

Namna gani unaweza kujibu ulizo hilo? Watu wengi wanawaza kama Mungu anafurahia vita. Wanawaza hivyo kwa sababu Mungu aliamuru watumishi wake fulani wa zamani wapigane vita; habari za Biblia zinahakikisha jambo hilo. Lakini, watu wengine wanasema kama Yesu, Mwana wa Mungu, alifundisha wanafunzi wake kupenda maadui wao. (Mathayo 5:43, 44) Kwa hiyo, wanafikiri kama wakati fulani mawazo ya Mungu juu ya vita yalibadilika na kama leo anachukia vita.

Unawaza namna gani? Mungu anafurahia vita? Kama jibu ni ndiyo, anaunga mukono upande gani katika vita za leo? Kupata majibu ya maulizo hayo kunaweza kukusaidia uchunguze mawazo yako juu ya vita. Kwa mufano, ikiwa ungejua kama Mungu anafurahia vita na anaunga mukono upande wenye unapenda katika vita fulani, pengine ungefurahi kuona ulichagua upande huo, na ungekuwa hakika kama upande wako utapata ushindi. Lakini, ungejisikia namna gani ukijua kama Mungu anaunga mukono upande mwengine katika vita? Pengine unaweza kuchunguza tena mawazo yako juu ya upande wenye ulichagua.

Lakini kuko jambo lingine la maana. Kujua mawazo ya Mungu juu ya vita kunaweza kubadilisha mawazo yako juu yake. Ikiwa uko kati ya mamilioni ya watu wenye wameteseka sana kwa sababu ya vita za wanadamu, kwa kweli, uko na lazima ya kujua jibu la ulizo hili: Mungu anachochea vita kama vile watu fulani wanaamini, anaachilia ao hata kuchochea mateso yenye kuletwa na vita, ao pengine hatende na hahangaikie hali ya watu wenye kuonewa?

Unaweza kushangaa kujua kama jibu lenye Biblia inatoa haliunge mukono hata wazo moja kati ya mawazo hayo. Tena, tangu zamani mupaka leo, mawazo ya Mungu juu ya vita hayajabadilika. Acha tuone mambo Biblia inasema juu ya namna Mungu aliona vita wakati wa zamani na wakati wa mitume, Yesu alipokuwa duniani. Hilo litatusaidia kujua namna Mungu anaona vita leo na ikiwa kutakuwa vita katika maisha ya watu wakati unaokuja.