Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Brais Seara/Moment via Getty Images

MUENDELEE KUKESHA!

Kipwa ya Nguvu na ya Kuendelea—Biblia Inasema Nini?

Kipwa ya Nguvu na ya Kuendelea—Biblia Inasema Nini?
  •   “China imeripoti kama hii mwaka njo ya mara ya tatu yenye kuwa na kipindi ya joto na kipwa ya nguvu sana.”—Tarehe 7, Mwezi wa 9, 2022, The Guardian.

  •   “Sehemu za Afrika zitapatwa na kipwa ya nguvu mu miaka tano za kufuatana.”—Tarehe 26, Mwezi wa 8, 2022, UN News.

  •   “Mu zaidi ya nusu ya Ulaya, kutakuwa kipwa yenye kuwa hatari, na inawezekana itakuwa ya nguvu sana mu kipindi ya miaka 500.”—Tarehe 23, Mwezi wa 8, 2022, BBC News.

 Watu wengi wenye elimu wanasema kama kipwa ya vile itaendelea na itakuwa hata nguvu sana. Kuko tumaini juu ya wakati yenye kuya? Biblia inasema nini?

Unabii wa Biblia Kuhusu Kipwa

 Biblia ilisemaka hivi kuhusu siku zetu:

  •   “Mahali pamoja kisha pengine kutakuwa upungufu wa chakula.”​—Luka 21:11.

 Mara mingi kipwa ya nguvu na ya kuendelea inaletaka upungufu wa chakula. Upungufu wa chakula wa vile unaletaka mateso na kifo. Na ile inatimiza unabii wa Biblia.​—Ufunuo 6:6, 8.

Juu ya nini kipwa inaendelea kuwa nguvu sana?

 Biblia inaonyesha sababu kubwa yenye inafanya kipwa iendelee kuwa nguvu sana. Inasema hivi:

  •   “Mwanadamu mwenye kutembea hana hata uwezo wa kuongoza hatua yake.”​—Yeremia 10:23.

 Ile inaonyesha kama wanadamu hawawezi “kuongoza hatua [zao],” ao kujitawala. Mara mingi wanakosaka kupanga mambo muzuri, ile inaletaka kipwa ya nguvu na ya kuendelea na inafanyaka hata maji ikosekane.

  •   Wanasayansi wengi wanasema kama mambo mbalimbali yenye wanadamu wanafanya inatokeza joto, na ile inafanya kipwa iongezeke mu dunia yote.

  •   Matendo ya watu wenye pupa na ya wale wenye kutia sheria bila kufikiria matokeo yenye ile italeta, inafanya pori, mazingira, na vitu vya maana vyenye kuwa mu dunia viharibike. Ile inaweza kufanya tukose mambo yenye tuko nayo lazima sawa vile maji.

 Lakini Biblia inaleta tumaini.

Kuko tumaini juu ya wakati yenye kuya?

 Biblia inaahidi kama Mungu atatosha magumu ya kukosa maji. Atafanya vile namna gani?

  1.  1. Mungu ‘ataharibu wale wenye wanaharibu dunia.’ (Ufunuo 11:18) Atatosha ile yenye inafanya maji ikosekane, ni kusema, watu wabaya, watu wenye pupa wenye matendo yao inaharibisha hali ya hewa.​—2 Timoteo 3:1, 2.

  2.  2. “Inchi yenye kukaushwa na joto itakuwa kama kiziwa cha maji chenye matete.” (Isaya 35:1, 6, 7) Mungu atageuza hii dunia yenye kuwa na kipwa ya nguvu na ya kuendelea na kuifanya kuwa paradiso mwenye mutakuwa maji yenye kuwa safi.

  3.  3. “Unatunza dunia, unaifanya izae kwa wingi na kuifanya ikuwe tajiri sana.” (Zaburi 65:9) Juu Mungu atabariki dunia, kutakuwa chakula mingi ya muzuri na maji yenye kuwa safi kwa ajili ya watu wote.