Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ismail Sen/Anadolu Agency via Getty Images

MUENDELEE KUKESHA!

Tetemeko Kubwa Sana ya Inchi Yenye Ilipiga Uturuki na Siria—Biblia Inasema Nini?

Tetemeko Kubwa Sana ya Inchi Yenye Ilipiga Uturuki na Siria—Biblia Inasema Nini?

 Siku ya Kwanza, tarehe 6 Mwezi wa 2, 2023, tetemeko kubwa sana ilipiga Uturuki na Siria.

  •    “Siku ya Kwanza, tetemeko kubwa sana ya inchi iliua watu zaidi ya 3 700 mu eneo kubwa ya Uturuki na mu kaskazini-mangaribi ya Siria. Ile ilitokea wakati kulikuwa baridi sana, na ile ilifanya hali ikuwe mubaya zaidi kwa maelfu ya watu wenye waliumia ao kupoteza nyumba zao. Ilikuwa pia nguvu zaidi kupata watu wenye waliokoka ile tetemeko.”—Reuters, tarehe 6 Mwezi wa 2, 2023.

 Roho inalumaka sana wakati tunapataka habari juu ya magumu ya vile. Jambo yenye tunaweza kufanya mu hali ya hivi, ni kumuomba Yehova a atusaidie juu yeye njo “Mungu wa faraja yote.” (2 Wakorinto 1:3) ‘Anatufariji kutoka katika Maandiko [ili] tukuwe na tumaini.’—Waroma 15:4.

 Mu Biblia, tunajifunza juu ya:

  •    Mambo yenye ilitabiriwa kuhusu matetemeko ya inchi.

  •    Fasi kwenye tunaweza kupata faraja na tumaini.

  •    Namna Mungu atamaliza mateso yote.

 Ili kujua mambo yenye Biblia inasema juu ya ile yote, soma habari zenye kufuata:

a Yehova njo jina ya pekee ya Mungu.—Zaburi 83:18.